AMBIA UTAWALA MPYA WA MAREKANI WAONDOE VIKWAZO VYA KIUCHUMI WAKATI DUNIA INAKABILIANA NA JANGA LA COVID-19
Kwa: Rais Joe Biden, Makamu wa Rais Kamala Harris na Wajumbe wa Bunge la Marekani
Tunawaandikia sababu tunahangaikishwa na athari za vikwazo vya Marekani dhidi ya nchinyingi zinazoumia sana sababu ya matokeo ya covid-19
Janga la Covid-19 duniani na kuzorota kwa uchumi ni changamoto kwa binadamuduniani kote. Ushirikiano wa kisayansi na kiteknologia na mshikamano vinahitajika sana kwasasa. Kinyume na hayo, utawala wa Trump umezidisha vita vya kiuchumi (“vikwazo”) dhidi yanchi nyingi duniani.
Tunawasihi muanze enzi mpya za uhusiano wa Marekani na Ulimwengu kwa kuondoavikwazo vyote vya kiuchumi
Vikwazo vya kiuchumi kutoka Marekani vimeathiri thuluthi moja ya wakazi dunianikatika mataifa 39
Hivi vikwazo vinazuia usafirishaji na ununuaji wa dawa za muhimu, vifaa vya kupima, vifaa vyakujikinga (PPE), chanjo, hata na vyakula vya msingi. Vikwazo pia husababisha ukosefu wamahitaji ya msingi, kutawanyika kwa uchumi, pesa kupoteza thamani yake kiholelela, njaaambazo zingeweza kuepukwa. magonjwa na ufukara vinavyosababisha maelfu ya vifo. Kila wakati ni maskini na mnyonge – vitoto, watoto, wenye magonjwa sugu na wazee – ndio haowanaopigwa kupita kiasi na athari za vikwazo.
Vikwazo si halali. Vikwazo ni kinyume na sheria ya kimataifa na Mkataba wa Umoja waMataifa. Vikwazo ni kosa la jinai dhidi ya binadamu vinavyotumiwa, kama sawa nguvu za kijeshi, kwa kupindua serikali ama vuguvugu za kiraia.
Marekani hutumia uwezo wake mkubwa wa kijeshi na kiuchumi kuonea nchi nyingine, mashirika ya kimataifa na makampuni kwa kusitisha uhusiano wa kawaida wa biashara zote nanchi zinazoshutumiwa, kama siyo mali zao kunyakuliwa, hata na kupigwa kijeshi.
Hatua ya kwanza kuelekea mabadiliko ni lazima iwe ya kukomesha siasa za vita vyakiuchumi. Tunawasihi musimamishe hivi vikwazo kwenye nchi zote bila kuchelewa nakuwanzisha upya uhusiano wa Marekani na Dunia.
Saini: https://sanctionskill.org/petition/
Kuna linki ya kusaini hii barua, Pamoja na jina lako, emaili, simu, shirika, chewo kama unasainiashirika.
Sanctions Kill.org imekuwa ikidhamini watumiaji wa mitandao, vikundi vyakutoa elimu na harakati nyingine pamoja na mikakati dhidi ya vikwazo kwanyakati hizi za janga la Covid-19, ikiwa ni pamoja na kutangaza mikakatiiliyochukuliwa na mashirika. Kama hatua mojawapo ya kampeni hizi, tunapongezajuhudi zinazoendelea za uhamasishaji na mafunzo. Tutaendelea kucangia mawazo kupitia info@sanctionskill.org